Jumamosi, 13 Desemba 2014

Maelfu Waandamana Washington na New York


Maelfu ya watu waandamana leo katika bara-bara za miji ya Washington na New York kupinga mauaji ya wanaume weusi wasiokuwa na silaha yaliyofanywa na polisi wa Marekani, ili kulitaka bunge lilinde wananchi.
Taarifa iliyotolewa na kiongozi wa kutetea haki za raia, Al Sharpton, ilieleza kuwa bunge linahitaji kuchukua hatua kubadilisha sheria na hali bara-barani.
Kati ya wataohudhuria maandamano hayo ni familia za Michael Brown, kijana aliyeuwawa katika jimbo la Missouri, na Eric Garner, ambaye alikufa wakati anakamatwa mjini New York.
Kesi za askari polisi waliohusika na vifo hivyo zilifutwa na kuzusha maandamano kote Marekani.

Undated photos of Michael Brown (left) and Eric Garner

.Juu ni picha za marehemu waliouawa kutoka kwa polisi nchini Marekani
A protester in Washington DC, 13 December "Mbingu inalia juu ya uvunjwaji wa haki za binadamu": Muandamanaji akiwa ameshika bango Jijini Washington DC
Protesters on a bus leaving New York for Washington DC, 13 December Mabasi yakiwa yamejaa Waandamanaji weusi kuelekea Jijini Washington na Miji mingine.
Protesters in Washington DC, 13 December "Hii tabia ikome leo": Ni msemo mwingine wa Waandamanaji.
A protester in Washington DC, 13 December  
Waandamanaji wakiendelea kupinga mauaji juu yao nchini Marekani.
Hapa inaonyesha Dunia haiwezi kukwepa desturi yake. Mara nyingi vitabu vya dini vimekuwa vikiandika kuwa binadamu wote ni sawa, lakini kwa miaka mingi sasa mwanadamu kuwa mweusi au hata kama atakuwa mweupe lakini asili yake ni Afrika amekaaliwa na mataifa ambayo watu wao wanadhani dunia hii iliumbwa kwa aajili yao.

0 maoni:

Chapisha Maoni