Jumanne, 10 Juni 2014

Kauli ya Profesa Jay Baada ya Diamond Kukosa tuzo za MTV MAMA

 


Diamond Platinumz alikuwa mshiriki kwenye kinyang’anyiro cha tuzo za MTV MAMA mwaka huu na kwa bahati mbaya hakushinda tuzo katika vipengele vyote viwili alivyokuwa akiwania.

Msanii mkongwe Profesa Jay ambaye anakumbukwa kwa kufanya mapinduzi kwenye muziki na kuwashawishi wazazi kuwaruhusu watoto wao kuimba kupitia kazi zake, amemuandikia ujumbe Diamond kupitia Instagram.
 
“Hapo ulipofika tayari wewe ni Mshindi mkubwa na Unayeipeperusha juu sana Bendera yetu ya TANZANIA, Wote tunaoitakia mema nchi yetu tuko nyuma yako Mpaka kieleweke, Usife moyo Kwani hii ni dalili njema ya kupata mafanikio zaidi na zaidi, Stay blessed and LET’S GO GET THEM!!!”

0 maoni:

Chapisha Maoni