Ijumaa, 6 Juni 2014

Machangudoa toka nchini Rwanda watiwa mbaroni mkoani Dodoma.....Mmoja wao ahukumiwa jela miaka miwili


Wanawake wanne raia wa Rwanda wametiwa mbaroni mjini Dodoma kutokana na kuingia nchini kinyemela na kujihusisha na biashara ya ukahaba. 
 
Watuhumiwa  watatu kati ya hao, Saidat  Umotoni (28), Asha Abimana (25) na Asia Umotoni  Wase (30), hii ni mara yao ya pili kukamatwa mjini hapa wakidaiwa kujihusisha na biashara hiyo. 
 
Mara ya kwanza ilikuwa Novemba mwaka jana ambapo wote  ( Asia, Asha na Saidat) baada ya kukamatwa, walirudishwa kwao baada ya kulipa faini. 
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana Kaimu Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma,  Proches Kuoko, alimtaja mwingine aliyekamatwa ni Chalote Uwase (28) ambaye ameshahukumiwa kifungo cha miaka miwili anachotumikia katika Gereza la Isanga, mjini hapa. 
 
Alisema wahamiaji hao wote kwa pamoja walikamatwa na maofisa wa kikosi cha Uhamiaji, baada ya kupata taarifa kwa kuwepo raia hao katika eneo la barabara ya Bahi ndani ya Manispaa ya Dodoma. 
 
Alisema wanawake hao walikamatwa  usiku kwenye mitaa hiyo huku wakiwa kwenye harakati za kutafuta  wateja na walipohojiwa wote kwa pamoja hawakuwa na hati ya kusafiria na kuishi hapa nchini na walizokuwanazo zilikuwa zimeisha muda wake wa matumizi. 
 
“Hata  walipopekuliwa,  walikutwa wakiwa na hati ya kusafiria iliyokuwa imeisha muda wake wa kuwawezesha kuishi hapa nchini na walipohojiwa zaidi walisema wao kazi yao ni uchangudoa,”alisema Kuoko.

0 maoni:

Chapisha Maoni