Alhamisi, 17 Aprili 2014

“NILIPONASA SASA SIPINDUI”….SHILOLE

STAA wa filamu na mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shishi Baby’ amefunguka kuwa amenasa vilivyo katika penzi la msanii mwenzake, Nuhu Mziwanda hatarajii kuachika.

Staa wa filamu na mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shishi Baby’ akiwa kwenye pozi la kimahaba na mpenzi wake aliyefahamika kwa jina la Nuhu Mziwanda

Akipiga stori na paparazi wetu, Shishi alisema yupo tayari kuolewa na Mziwanda kwani anampenda na ndiyo ubavu wake kutokana na vile ambavyo amekuwa akimwonesha mapenzi ya kweli tofauti na wapenzi wake wote waliopita.

‘Shishi Baby’akiwa kwenye pozi na Nuhu Mziwanda.
“Huyu ndiye shemeji yenu, ndiye mume wangu mtarajiwa, ninampenda na yeye ananipenda kwa hiyo Mungu akijalia soon tutakamilisha taratibu za ndoa,’’ alisema Shishi Baby.

0 maoni:

Chapisha Maoni